Wachezaji watano wa kulipwa waitwa katika kikosi cha Misri
Kocha wa timu ya taifa ya Misri Hossam El-Badry amewaita kikosini wachezaji watano wa kulipwa kwa mechi za mwezi Novemba kufuzu kwa kombe la Afcon mwaka 20121.
Misri ambao ni mabingwa mara 7 wa kombe hilo la Afcon wameanza vibaya harakati za kufuzu kutoka kundi G wakiwa na pointi 2 baada ya kutoka sare dhidi ya Kenya na Comoros.
Wanandinga wa kulipwa walijumuishwa kikosini ni Mohamed Salah wa Liverpool , Mohamed Elneny wa Arsenal, Ahmed Hegazi wa Westbromwich Albion, Mahmoud Trezeguet wa Aston Villa, na Ahmed Hassan Kouka wa Olympiacos ya Ugiriki.
Misri watapambana na Togo nyumbani na ugenini mwezi ujao kuwania tiketi ya kwenda Afcon mwaka ujao.