Timu ya Uganda maarufu kama Hippos imeanza vyema mechi za kundi A katika mashindano ya kuwania kombe la AFCON kwa chipukizi walio chini ya umri wa miaka 20 baada ya kuwacharaza Msumbiji mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa Jumatatu alasiri nchini Mauritania .
Mshambulizi wa klabu ya Police Derrick Kakooza alipachika bao la kwanza dakika ya 57 kupitia penati kabla ya kiungo wa KCCA Steven Serrwada dakika 4 kabla ya kipenga cha mwisho huku ushindi huo ukiwaweka katika nafais nzuri ya kutinga robo fainali wakiongoza kundi hilo kwa alama 3 sawa na Cameroon kuelekea kwa mechi kati ya timu hizo mbili Jumatano hiii.
Mashindano hayo yanashirikisha mataifa 12 huku fainali yake ikipigwa tarehe 6 mwezi ujao.