Kansella Angela Merkel wa Ujerumani ameonya kuhusu kipindi kigumu na kirefu cha majira ya baridi,huku akitetea kurejelewa tena kwa sheria za kufunga shughuli nchini humo kuzuia kusambaa kwa ugonjwa wa Covid-19.
Merkel alionywa na wabunge wa mrengo wa kulia alipotangaza kurejelewa kwa sheria hizo katika bunge.
Maafisa wa afya wamesema kuwa takriban watu 89 walifariki nchini humo siku ya alhamisi kutokana na ugonjwa huo,huku wengine 16,774 wakiambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
Hata hivyo sheria hizo si kali kuliko zile zilizotangazwa na taifa la Ufaransa ambalo lilifunga baa,migahawa na majumba ya mazoezi ya misuli na ya wasanii.
Ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huo barani ulaya limesababisha mataifa husika kutangaza sheria kali zaidi.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alitangaza sheria mpya za kukabiliana na janga hilo baada ya vifo kutokana na ugonjwa huo kuongezeka kwa kiwango kikubwa tangu mwezi Aprili.
Siku ya Alhamisi taifa hilo lilirekodi visa 47,637 vipya vya ugonjwa huo,ikilinganishwa na visa 36,437 vya siku iliotangulia na vifo vya watu 235 siku ya jumatano.