Kocha mkuu wa timu ya taifa ya soka ya wanawake Harambee Starlets , David Ouma ametangaza kikosi cha awali kwa mech ya kirafiki dhidi ya Zambia tarehe 24 mwezi huu.
Martha Amnyolet aliyeshiriki mashindano ya CECAFA mwaka 2018 nchini Rwanda amerejeshwa kikosini wakati pia mabeki
Dorcas Shikobe wa Thika Queens na Foscah Nashivanga wakiwania nafasi ya beki kisiki.
Timu hiyo itaingia kambini tarehe 15 mwezi huu kwa maandalizi kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Zambia maarufu kama Shepolopolo mjini Lusaka April 24.
Kikosi cha awali kilichotajwa kinawajumuisha:-
Makipa
Annette Kundu (AEL Champions) , Valentine Khwaka (Mathare United Ladies), Pauline Muthakye (Kibera Soccer Ladies), Judith Osimbo
Mabeki
Ruth Ingosi (AEL Champions), Quinter Owiti, Dorcas Shikobe (Thika Queens), Foscah Nashivanga, Nelly Sawe (Thika Queens), Leah, Vivian Nasaka (Vihiga Queens), Juliet Andipo (Kayole Starlet), Lucy
Viungo
Lillian Mmboga(Kibera Soccer Ladies), Vivian Corazone Aquino (Gaspo Women), Sheryl Angachi (Gaspo Women), Lydia Akoth (Thika Queens), Laventine Lihemo (Kibera Soccer Ladies), Topister Situma (Vihiga Queens), Puren Alukwe (Zetech Sparks), Diana Wacera (Gaspo Women), Rael Kamanda (Makolanders), Janet Bundi (Vihiga Queens), Siliya Rasoha (Ulinzi Starlets), Rachael Muema (Thika Queens), Martha Amnyolet
Washambulizi
Mwanahalima Adam (Thika Queens), Mercy Airo (Gaspo Women), Gily Okumu, Faith