Tag: Fkf Premier league
Bidco United walisajili ushindi wa kwanza ligini msimu huu, baada ya kuilaza Vihiga United bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu Fkf iliyochezwa Jumapili alasiri katika uchanjaa wa Moi kaunti ya Kisumu.
Bao la pekee na la ushindi kwa Bidco iliyopandishwa ngazi msimu huu lilipachikwa na Nelson Chieta kunako dakika ya 37.
Katika mechi nyingine iliyopigwa kiwarani Kasarani Tusker Fc walitoka sare ya bao 1-1 na wageni Sofapaka Ellie Asieche akifunga bao la Sofapaka dakika ya 6 kabla Tusker kurejea mchezoni kwa bao la Luke Namanda dakika ya 25.
Katika uga wa Utalii Wazito Fc iliwapachika Nairobi sity stars magoli 2-1 huku Bandari pia ikiwazima Western Stima mabao yayo hayo 2-1 katika uga wa Mbaraki.
Timu za Mathae United na Zoo fc hazijacheza mechi za ufunguzi huku Gor Mahia wakicheza mechi mbili pekee wakati timu nyingi zikiwa zimesakata michuano 6 kila moja.
Ulinzi watoshana nguvu na Sharks
Ulinzi Stars na Kariobangi Sharks waliumiza nyasi bila lengo maalum baada ya kuambulia sare tasa Jumamosi alasiri katika mojawapo wa mechi mbili za ligi kuu iliyochezwa uwanjani Kasarani.
Katika uwanja wa Bukhungu pia jumamosi wenyeji Nzoia Sugar walitoka sare kapa dhidi ya Kakamega Homeboyz .
Ratiba ya Jumapili
1. Wazito vs Nairobi City Stars (Utalii Grounds, 3 pm)
2. Tusker FC vs Sofapaka (Kasarani Stadium, 3 pm)
3. Vihiga United vs Bidco United (Mumias Sports Complex, 3 pm)
4. Bandari vs Western Stima ( Mbaraki Grounds, 3 pm)
Shirikisho la kandanda nchini FKF limepatwa na pigo baada ya mahakama ya kutatua migogoro michezoni nchini SDT kuamuru kurejeshwa ligini timu za Mathare United na Zoo Fc kusubiri uamuzi wa kesi iliyowasilishwa dhidi ya FKF na vialbu hivyo viwili wiki ijayo.
Mwenyekiti wa Mahakama hiyo maarufu kama SDT John Ohaga ametoa uamuzi huo mapema Alhamisi wa kuzirejesha timu hizo mbili kwenye ligi pamoja na kubatilisha uamuzi wa awali wa FKF wa kutamatisha kandarasi za wachezaji wote wa klabu hizo mbili .
Pia jaji Ohaga ameagiza Fkf iliruhusu wachezaji na maafisa wa vilabu hivyo kufanyiwa vipimo vya COVID 19 sawa na vilabu vingine saa 72 kabla ya kuanza mechi zao za ligi kuu .
Baraza kuu la FKF likikutana Desemba 9 na kuamuru kuzipiga marufuku timu hizo hadi pale zitakaposaini mkataba huo wa Star Times.
FKF ilizipiga marufuku timu hizo kushiriki ligi kuu ya FKF baada ya kudinda kusaini mkataba wa Star Times ambao ungewezesha mechi za timu hizo kupeperushwa mbashara na runinga hiyo ya China .
Shirikisho hilo pia linamchunguza mwenyekiti wa Gor Mahia Ambrose Rachier baada yake kaundika barua kwa Star Times kuondoa barua ya kwanza iliyoandikwa na aliyekuwa katibu mkuu Sam Ochola kusaini mkataba huo .
Zoo FC vs. Kenya Football Federation – Order (17 Dec 2020)
Mkataba wa FKF na Star Times umeibua hisia kali huku vilabu vya Ulinzi Stars,Mathare United ,Gor Mahia na Zoo Fc vikiupinga kwa kukiuka haki zao hatua iliyochangia kupigwa marufuku na kutimuliwa ligini kwa Mathare United na Zoo Fc .
Timu za Mathare na Zoo zilizuiwa kucheza mechi zao za kufungua msimu wa ligi wiki jana wakati Gor na Ulinzi wakiwa tayari wamecheza mechi 2 na moja mtawalia katika ligi kuu.
Mahakama ya SDT itakutana wiki ijayo kusikiza kesi hiyo na kutoa maelekezo zaidi huku ligi ya FKF ikiangia mechi za mzunguko wa nne mwishoni mwa juma hili.
Kilabu ya Zoo Fc imewasilisha kesi ya dharura katika mahakama ya kutatua migogoro michezoni SDT kutaka iruhusiwe kucheza mechi zake ligi kuu ya Fkf ,bila kupeperushwa kupitia runinga ya Star Times baada ya kudinda kusaini mkataba huo .
Zoo fc yenye makao yake katika kaunti ya Kericho imesusia kucheza mechi zake mbili za ufunguzi za ligi kuu kutokana na kutokubaliana na mkataba huo, huku ikijiunga na timu za Ulinzi Stars,Mathare United na Gor Mahia ambazo zimesusia kusaini pia mkataba huo wakidai una vipengee vyenye utata.
Mwenyekiti wa Zoo fc Ken Ochieng’ amemtaka Rais wa FKF kukomesha vitisho na kuonyesha mfano mwema wa uongozi akisema hawako tayari kuachilia haki zao za runinga kwa shirikisho.
“Vitisho na unyanyasi havina nafasi haswa wakati wa swala linalohusu haki za matangazo ya runinga kwa kilabu ,tumeambiwa tupeane haki zetu kwa miaka saba huku tukilipwa kiwango cha chini cha pesa na hakuna kipengee cha kujiondoa ukisha Saini mkataba huo ,ni mkataba ambao hauna faida yoyote kiuchumi kwa timu”akasema Ochieng’
Timu zote zilizotia saini mkataba huo zimepokea shilingi milioni 2 .
Fkf imeratibu timu za Gor Mahia na Ulinzi Stars kucheza mechi yao ya ufunguzi Jumamosi hii huku Zoo Fc na Mathare united zikiachwa nje.
Baraza kuu la Fkf linatarajiwa kukutana kuamua hatima ya vilabu hivyo vine huku ikidokezwa kuwa huenda timu hizo zikatimuliwa ligini.
Miamba wa soka nchini Kenya Afc Leopards waliendeleza msururu wa matokeo mazuri kwa kulilaza Bidco United mabao 2-0 katika mechi ya ligi kuu iliyosakatwa Jumapili Jioni katika uwanja wa Kasarani.
Leopards walihitaji mabao 2 ya mshambulizi Elvis Rupia kunako kipindi cha pili ili kuwatema Bidco waliopandishwa ngazi ligini msimu huu na kudumisha rekodi ya asilimia 100 baada ya michuano miwili kwani pia wakikuwa wameilaza Tusker Fc mabao 2-1 katika pambano la ufunguzi.
Sofapaka wakiwa Kilifi waliwateketeza Western Stima mabao 3-1 ,Ellie Asieche akicheka na nyavu mara mbili ,moja kila kipindi huku naye Kepha Aswani akafunga kazi kwa Batoto Ba Mungu kwa goli la 3 huku lile la maliwazo kwa wageni Stima likifungwa na Samuel Odhiambo.
Huo ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Sofapaka waliopoteza pambano la ufunguzi bao 1-0 ugenini kwa Bandari Fc.
Kwenye matokeo mengine wana Mvinyo Tusker watazidi kusubiri ushindi wa kwanza ligi, baada ya kukabwa koo na Bandari Fc kwa kutoka sare kapa huku Kakamega Homeboyz wakishindwa kutamba nyumbani na kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Posta Rangers.
Leopards wanaongoza jedwali kwa pointi 6 sawia na KCB baada ya mechi mbili .
KCB FC na Wazito FC zaibuka kidedea
Baada ya kuambulia kichapo katika mechi za raundi ya kwanza ya ligi kuu wiki jana,timu ya Wazito Fc imesajili ushindi wa kwanza leo kwa kuwalemea Vihiga United mabao 3-1 katika mchuano wa ligi kuu uliosakatwa Ijumaa alasiri katika uwanja wa kaunti ya Narok,.
Wazito walichukua uongozi wa pambano hilo kunako dakika ya 12 ya mchezo kupitia kwa mshambulizi Boniface Omondi kabla ya beki Dennis Ng’ang’a kuongeza la pili robo saa baade huku wakiongoza 2-0 kufikia mapumziko.
Mshambulizi wa zamani Leopards Wyvone Isuza aliongeza bao la tatu katika dakika ya 54 lakini Norman Werunga akapachika goli la kufutia machozi kwa wageni katika dakika ya 64.
Iilikuwa mechi ya pili mtawalia kwa Vihiga united kupoteza tangu warejee kwenye ligi kuu ,baada ya kuangushwa pia kwa bao moja kwa sifuri na Kakamega Homeboyz wiki jana.
Wahifadhi hela KCB waliibwaga Nairobi City Stars goli 1-0 katika mchuano mwingine wa Ijumaa uwanjani Kasarani.
Bao la pekee na la ushindi kwa Kcb ilikipachikwa kimiani na Difenda Henry Onyango kunako dakika ya 43.
Mechi mbili zaidi za mzunguko wa pili wa ligi kuu kupigwa Jumamosi Nzoia Sugar wakiwaalika Kariobangi Sharks uwanjani Sudi kuanzia saa tisa huku Tusker Fc na Bandari fc wakimenyana uwanjani Kasarani kaunzia saa tisa pia.
Shirikisho la kandanda nchini Fkf litaziadhibu timu ambazo hazitasaini mkataba wa kupeperusha mechi za ligi kuu inayotazamiwa kuanza Jumamosi hii.
Akizungumza na wanahabari jijini Nairobi mapema Alhamisi ,mwenyekiti wa Fkf Nick Mwendwa amesuta vilabu vinne ambavyo havijasaini mkataba huo wa matangazo ya runinga akisisitiza kuwa vimepewa nafasi ya mwisho kubatilisha misimamo yao mikali na kuruhusu ligi kuanza bila tashwishwi.
“Sisi tuko tayari kuanza ligi Jumamosi bila hizo timu nne ambazo hazijasaini mkataba huo,lakini pia tunawapa nafasi ya kufikiria upya kuhusu uamuzi wao ,la sivyo tutachukua hatua kama shirikisho wiki ijayo,hakuna vile timu hizo zitazuia ligi kuanza”akasema Mwendwa
Mwendwa amekariri kuwa haki zote za ligi ya Kenya zinamilikiwa shirikisho na wala sio za vilabu inavyodaiwa .
“Fkf ndio wameliki wa haki zote za soka humu nchini na pia ligi ya Fkf Premier League,kwa hivyo tusidanganyane ,si bado tunaomba timu za Zoo Fc,Gor Mahia ,Mathare United na Ulinzi Stars kutafakari na kubadilisha msimamo wao ligi ianze vijana wapate doo”akaongeza Mwendwa
Fkf imezindua mkataba wa miaka 7 na kampuni ya Star Times ya kutoka China ili kupeperusha mechi za ligi kuu ambapo inatarajiwa kuwa angaa mechi 100 zitarushwa kwenye runinga kila msimu .
Hata hivyo kwenye mahojiano na Kbc kwa njia ya simu mwenyekiti wa Gor Mahia Ambrose Rachier ameapa kuelekea mahakamani kusimamisha mkataba huo wa runinga na kupinga hatua ya Fkf Kumiliki haki zote za vilabu.
“Mimi kwa sasa sina wakati wa kujibizana na Fkf lakini nitafuata mkondo wa sheria ambapo nitaelekea mahakamani kutaka kusimamishwa kwa mkataba huo kwa sababu haki za vilabu hazipaswi kutwaliwa na shirikisho”akasema Rachier
Utata huo huenda ukaibuka mvutano mkubwa kwenye ligi kuu ambayo iliratibiwa kuanza Jumamosi hii ambapo jumla ya mechi 3 zimeratibiwa kupeperushwa kupitia Runinga ya Star Times.
Kilabu cha Gor Mahia kimempiga marufuku katibu mkuu wake Sam Ocholla kwa kusaini barua ya mkataba wa kupeperusha mechi la ligi kuu FKF baina ya kampuni ya Star Time na FKF.
Akitangaza kumpiga marufuku ya Ocholla,mwenyekiti wa Gor Ambrose Rachier amesema kuwa ilikuwa kinyume cha sheria kwa katibu huyo kusaini barua hiyo bila kushauri usimamizi mkuu wa timu na tayari wameandika barua kwa kampuni ya Stars Times kujitenga na mwafaka huo.
Kulingana na Rachier uamuzi huo sio wa kuchukuliwa na mtu binafsi.
“kulingana na katiba ya kilabu ibara ya 15 mkataba wowote kama huo unaweza ukatiwa saini tu mwenyekiti wa timu,na hatuko tayari kuuza haki zetu kwa huo mkataba kwani hatujaona kandarasi kati ya FKF na Stars Times ndio maana hatukubaliani na mkataba huo”akasema Rachier
Rachier amesisitiza kuwa wako tayari kushiriki ligi kuu inayotazamiwa kuanza tarehe 28 mwezi huu,lakini hawatauza haki zao kwa kusaini mkataba huo.
”Sisi tuko tayari kaunza ligi lakini kile hatutafanya ni kuuza haki zetu,kile FKF wanafanya ni kinyume cha sheria kwa vilabu kupokonywa haki zao”akaongeza Rachier
Hata hivyo Ochola ameitisha kikao na wanahabari Jumatano kujitetea akidokeza kuwa uamuzi huo wa kusaini barua ya mkataba aliuafikia baada ya kupewa idhini na baraza kuu la kilabu.
Kampuni ya Star Times yenye makao yake nchini China ilisaini mkataba wa miaka 7 na Fkf kumiliki haki zote za matangazo ya runinga ya ligi kuu ,mechi za timu za taifa za wanaume na wanawake na mechi 30 za ligi ya NSL.
Vilabu vinne vimedinda kusaini mkataba huo vikiwemo Gor Mahia,Ulinzi Stars ,Mathare United na Zoo Fc kwa misingi ya kutofahamu yaliyimo kwenye kandarasi hiyo.
Ligi ya Nsl kung’oa nanga Disemba 5
Kulingana na Fkf ligi hiyo imesukumwa mbele kwa wiki moja kutoka tarehe ya awali, baada ya ligi kuu ya FKF kuahirishwa kutoka Novemba 20 hadi Novemba 27.
Ligi ya NSL itashirikisha timu 17 msimu huu kinyume na 19 za msimu jana baada ya Chemilil Sugar Fc na Ushuru Fc kuvunjiliwa mbali kutokana na ukosefu wa pesa na hivyo basi kutoa fursa kwa Silibwet Leos Fc,Soy United na Mwatate United Fc kupandishwa ngazi kucheza ligi hiyo.
Timu mbili bora kutoka ligi hiyo hupandishwa ngazi kucheza ligi kuu ya FKF huku ile ya tatu ikicheza mchujo dhidi ya timu ya 16 katika ligi kuu ambapo mshindi hushiriki ligi kuu.
Wachezaji wa vilabu vyote vya ligi kuu wanapitia vipimo vya Covid 19 kwa mjibu wa matakwa ya serikali kabla ya ligi kuanza rasmi.
Ligi kuuu ya Fkf msimu wa mwaka 2020-2021 uantazamiwa kuanza mwishoni mwa juma hili kwa mechi tatu Afc Leopards wakipambana na Posta Rangers katika uwanja wa Nyay,o huku Mathare united ikifungua dimba dhidi ya Kakamega Homeboyz nao Bandari Fc waanze msimu nyumbanio dhidi ya Zoo Fc.