Rais Uhuru Kenyatta amezindua mpango wa kibiashara wa MbeleNaBiz wa kuwatuza wajasiria mali chipukizi na uzinduzi wa mpango makhsusi wa hazina ya vijana wa mwaka 2020-2024.
Akisimamia uzinduzi huo katika Uwanja wa Michezo wa Moi Kasarani Jijini Nairobi, Rais Kenyatta amesema serikali itatenga shilingi bilioni 1.3 za kufadhili uchumi wa vijana wa taifa hili.
Kulingana na Rais, kati ya pesa hizo, shilingi milioni 900 zitatolewa kwa wajasiriamali 250 kama ruzuku.
“Jumla ya shilingi milioni 900 zitapewa
Rais pia ametumia fursa hiyo kuhimiza vijana kuunga mkono mpango wa maridhiano wa BBI ambao tayari umeungwa mkono na mabunge 40 ya kaunti.
Amesema kupitishwa kwa mpango huo kutawawezesha vijana kupata pesa na kuhakikisha rasili mali zaidi zinawasilishwa katika maeneo ya magatuzi ili kufadhili maendeleo.