Simba Sports club wameweka hai matumaini ya kutinga robo fainali ya kombe la ligi ya mabingwa Afrika baada ya kuwachuna mabingwa watetzi Al Ahly bao 1-0 katika mkwangurano uliosakatwa Jumanne alasiri katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Daresalaam Tanzania.
Bao la pekee na la ushindi kwa mnyama simba lilipachikwa kimiani na kiungo wa Msumbiji Luis Muquissone kunako dakika ya 39 na kudumu hadi kipenga cha mwisho.
Kichapo cha Al Ahly kilikuwa cha kwanza katika ligi ya mabingwa Afrika baada ya zaidi ya msimu mmoja .
Uwanja wa Mkapa ulifurika hadi pomoni wakati wa mechi hiyo baada ya tiketi zote za mechi kuuzwa .
Ushindi huo unaweweka Simba uongozini pa kundi A kwa alama 6 baada ya mechi 2 kufuatia ushindi wa goli 1-0 ugenini mjini Kinsasha dhidi ya As Vita katika pambano la ufunguzi .
Mnyama Simba ataanza matayarisho kwa ziara ya Khartoum mwishoni mwa juma hili dhidi ya El Merreikh ya Sudan huku wakihitaji angaa ushindi katika mechi mbili kati ya 4 zilisozalia ili kutinga kwota fainali kwa mara ya kwanza.
Mshambulizi wa Harambee Stars Michael Olunga alicheza dakika 46 kabla ya kuondolewa uwanjani katika ushinde wa timu yake ya Al Duhail Sc wa bao 1 na mabingwa wa Afrika Al Ahly katika kwota fainali ya kombe la dunia baina ya vilabu katika uwanja wa Education City Stadium mjini Al Rayyan nchini Qatar Alhamisi usiku.
Ilikuwa mechi ya kwanza kwa Olunga kucheza katika fainali hizo za kombe la dunia akiwakilisha mabingwa hao watetezi wa ligi kuu nchini Qatar tangu ajiunge nao mwezi uliopita kutoka kashiwa Reysol ya Japan.
Tobwe la Hussein El Shahat kunako dakika ya 30 liliotosha kuwapa Ahly maarufu Red Devils kutoka Misri ushindi huo ambao uliwafuzisha kwa nusu fainali watakapochuana na mabingwa wa ulaya Bayern Munich Februari 8 wakilenga kuwa timu ya pili ya Afrika kucheza fainali ya kombe hilo baada ya TP Mazembe ya Jamhuri ya demokrasia ya Congo.
Katika mechi nyingi ya robo fainali mabingwa wa Marekani Kaskazini Tigres UNL ya Mexico waliibandua Ulsan Hyundai ya Korea Kusini mabao 2-1 na kufuzu kwa nusu fainali kuchuana na mabingwa wa Amerika Kusini Palmeiras ya Brazil .
Al Duhail watarejea uwanjani dhidi ya mabingwa wa Asia Ulsan kuwania nafasi ya 5 na 6 tarehe 7 kabla ya fainali ya tarehe 11 mwezi huu.
Mashindano hayo hushirikisha mabingwa wa kila bara na huandaliwa kila mwaka .
Miamba kadhaa wa soka barani Afrika walifuzu kwa hatua ya makundi kuwania taji ya ligi ya mabingwa Afrika kufuatia mechi za marudio ya michujo ya pili iliyosakatwa Jumanne .
Teungueth
Mabingwa mara 9 wa kombe hilo na mabingwa watetezi Al Ahly kutoka Misri walitinga hatua ya makundi kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-0 baada ya kuwacharaza SONIDEP ya Niger magoli 4-0 katika mkumbo wa pili uliosakatwa mjini Cairo Misri Jumanne usiku.
Al Ahly
Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini kusini maarufu kama Masandawana walipata ushindi wa jumla wa mabao 5-1 dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana baada ya kuwapiga wageni Jwaneng mabao 3-1 Jumanne.
Mamelodi Sundowns
Kaizer Chiefs ukipenda Amakhosi ,wakicheza ugenini Luanda walikosa heshima na kuwapiga kumbo Premeiro De Agosto bao 1-0 na kufuzu kwa makundi ya kombe hilo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 24 ,huku limbukeni Teungueth ambao ni mabingwa wa Senegal wakiwaduwaza miamba Raja Casablanca ya Moroko walipowabandua kupitia penati 3-1 kufuatia sare tasa.
Kaizer Chiefs
Timu nyingine iliyotinga awamu ya makundi kupitia kupewa ushindi wa ubwete kufuatia kujiondoa kwa wapinzani wao ni Zamalek kutoka Misri waliocheza hadi fainali ya mwaka jana,waliopewa ushindi baada ya Gazzelle ya Chad kujiondoa.
Mechi zaidi kupigwa Jumatano ambapo ratiba kamili ya timu 16 kucheza hatua ya makundi itabainika.
Kilabu ya Al Ahly ukipenda Red Devils ilinyakua kombe la ligi ya mabingwa barani Afrika kwa mara ya 9 Ijumaa usiku katika uwanja wa Cairo International baada ya kuwalemea Zamalek kwenye fainali iliyokuwa derby ya Cairo.
Mohammed Madgy Afsha aliwafungia Ahly bao la ushindi dakika nne kabla ya mechi kukamilika baada ya pambano hilo kuonekana kama lingeamuliwa katika muda wa ziada.
Kiungo Amr Soleya alifungua ukurasa kwa magoli katika mechi hiyo iliyokuwa ya kusisimua alipounganisha tobwe la Ali Maloul katika dakika ya 6 na kuwaweka Ahly kifua mbele na kuwafanya Ahly kutawala mechi kwa muda tokea mwanzoni mwa mechi.
Hata hivyo kiungo mkongwe Shikabala alitumia tajriba yake na kufyatua kombora kali mithili ya fataki, akiunganisha pasi ya Achraf Bencharki na kumwacha kipa wa Ahly Mohammed El Shanawy akiduwaa asiwe na la kufanya na kipindi cha kwanza kukatika kwa sare ya 1-1.
Licha ya kujaribu kurejesha bao hilo ,muda uliwapa kisogo Zamalek huku Ahly wakijihami zaidi baada ya kocha Pitso Mosimane kufanya mabadiliko ya kiufundi akiwaondoa washambulizi na viungo na kuwajumuisha mabeki na kushikilia uongozi huo hadi kipenga cha mwisho.
Idadi ndogo ya mashabiki waliohudhuria fainali hiyo walipata burudani ya kipee na kufurika uwanjani kushangilia ushindi wa Ahly ikiwa pia historia kwa maya kwanza ambapo fainali hiyo inashirikisha timu hizo za Misri.
Mosimane pia aliingia kwenye madaftari ya kumbukumbu kwa kuishinda Zamalek kwa mara ya pili katika fainali ya kombe hilo ,baada ya kuwashinda na kunyakua kombe hilo kwa mara ya kwanza akiwa na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini mwaka 2016.
Ahly ndio timu iliyoshinda kombe hilo mara nyingi ikiwa mara 9 na la kwanza tangu mwaka 2013 , huku vilabu kutokea Misri vikinyakua jumla ya vikombe 15 vya ligi ya mabingwa .
Fainali ya ligi ya mabingwa barani afrika itasakatwa Ijumaa usiku katika uwanja wa Cairo International ,ikiwa derby ya Cairo baina ya mabingwa mara 8 Al Ahly dhidi ya Zamalek kuanzia saa nne usiku.
Timu hizo zitakutana kwa mara ya 9 katika kombe hilo la ligi ya mabingwa, Ahly wakiibuka washindi mara 5 na nyingine 3 kuishia sare, lakini zote zikiwa aidha mechi za makundi au nusu fainali.
Itakuwa mara ya kwanza kwa timu hizo kukutana katika fainali ya kombe hilo zikiwania dola milioni 2 nukta 5 na fursa ya kucheza kombe la dunia baina ya vilabu.
Katika mechi za nyumbani timu hizo zimepambana mara 215 Ahly maarufu kama Red Devils wakishinda mechi 91 ,huku Zamalek wajulikanao kama White Knights wakisajili ushindi kwenye michuano 50 na kurekodi sare 74 .
Ahly wamenyakua ligi ya mabingwa mara 8 ikiwa timu iliyoshinda taji hiyo mara nyingi zaidi na kushinda mataji 4 ya kombe la shirikisho,4 ya African Cup winners cup na lile la super cup mara 4 kwa jumla wakiwa na vikombe 19 vya Afrika.
Hata hivyo Red Devils wamekawia tangu mwaka 2014 ikiwa mara ya mwisho kwao kunyakua kombe la shirikisho huku yale ya ligi ya mabingwa yakiwakwepa na ndiyo timu iliyokawia muda mrefu zaidi kabla ya kushinda kombe la ligi ya mabingwa.
Al Ahly wakiwa mazoezini
Upande wa pili wa sarafu Zamalek wamewshinda mataji matano ya ligi ya mabingwa ,4 ya Super Cup na moja ya shirikisho na nyingine moja ya African cup winners cup wakiwa na vikombe 11 vya Afrika.
Zamalek iliibuka ya pili katika kundi A nyuma ya Toupiza Mazembe kabla ya kuwatema waliokuwa mabingwa matetezi Esperance ya Tunisia jumla ya mabao 3-2 katika robo fainali na kuwabandua Raja Casablanca jumla ya mabao 4-1 kwenye nusu fainali.
Ahly nao waliibuka wapili kundini B nyuma ya Etoile du Sahel kabla ya kuibwaga Mamelodi Sundowns magoli 2-1 katika kwota fainali na hatimaye kuwadhalilisha mabingwa wa Moroko Wydad Casblanca kwa kuwalabua mabao 5-1 katika nusu fainali.
Kocha wa Afrika Kusini Pitso Mosimane alishika hatamu za kuwanoa Ahly mwezi Septemba mwaka huu akitokea Mamelodi Sundowns ya nyumbani ambao alishinda nao kombe hilo la ligi ya mabingwa mara moja .
Jaime Pacheco wa kutoka Ureno alirejea kuwafunza Zamalek pia mwezi Septemba mwaka huu akiwa hana kazi tangu aigure timu hiyo mwaka 2014.
Zamalek wakiwa mazoezini
Misri itanyakua kombe hilo la ligi ya mabingwa Ijumaa usiku kwa mara ya 15 likiwa taifa pekee kunyakua mataji mengi zaidi kwani awali Zamalek wameibuka mabingwa mara 5 nao Ahly wakashinda mara 8 wakati Ismaily ikishinda kombe moja.
Ahly wameshinda kombe la ligi ya mabingwa mwaka 1982 ,1987,2001,2005,2006,2008,2012 na 2013 na kupoteza fainali mara 4 ,ya mwisho ikiwa mwaka 2018.
Zamalek wametawazwa mabingwa miaka ya 1984 ,1986 ,1993,1996 na 2002 na kushindwa katika fainali mara mbili ya mwisho ikiwa 1996.
Fainali hiyo kati ya Al Ahly na Zamalek itapeperushwa mbashara kupitia KBC Channel one kuanzia saa nne usiku
Zamelek walijikatia tiketi kucheza derby ya fainali kuwania kombe la ligi ya mabingwa barani Afrika kufuatia ushindi mkubwa wamabao 3-1 dhidi ya Raja Casablanca Jumatano usiku katika marudio ya nusu fainali ugani Cairo.
Zamalek ambao wamenyakua kombe hilo mara 5, walikuwa na wakati mgumu huku wageni Raja wakichukua uongozi kunako dakika ya 61 kupitia kwa Ben Malango, kabla ya Ferjani Sassi ,kusawazisha naye Mostafa Mohammed akafunga mabao mawili ya haraka katika dakika za 84 na 87 mtawalia na kuwapa wenyeji fursa ya kuwania kombe la 6.
Ni mara ya kwanza kwa Zamalek maarufu kama White Nights kucheza fainali hiyo tangu wapoteze mwaka 2016 kwa Mamelodi Sundowns.
Zamalek walifuzu kwa fainali hiyo ya Novemba 27 dhidi ya Al Ahly katika uwanja wa Borg El Arab mjini Alexandria ,baada ya kuwapiku Raja Casablanca kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-1 kufuatia ushindi wa bao 1-0 katika duru ya kwanza ya nusu fainali.
Ahly wametwaa kombe hilo mara 8 na walitinga fainali kufuatia ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Wydad Casablanca ya Moroko kumaanisha kuwa kombe hilo litanyakuliwa na timu ya Misri.
Mshindi wa fainali ya Novemba 27 atatuzwa kombe dola milioni 2 nukta 5 za Marekani na nafasi ya kucheza fainali ya kombe la dunia baina ya vilabu mwezi ujao nchini Qatar.
Al Ahly walinyakua ubingwa wa ligi kuu nchini Misri kwa mara ya 42 mwishoni mwa wiki iliyopita huku msimu ukikamilika .
Kocha wa Ahly Pitso Mosimane aliendeleza matokeo bora katika majukumu yake mapya na miamba hao wakiipiga Talaea El Geish mabao 3-0 na kufunga msimu kwa pointi 89.
Walid Soliman , Geraldo na Mahmoud Kahraba walipachika mabao hayo ya Ahly ambao wameshinda mechi 28 kati ya 34 walizocheza huku wakipiga sare tano na kushindwa mchuano mmoja pekee.
Kwa jumla Ahly maarufu kama Red Devils wamefungwa mabao manane na kuandikisha rekodi ya kuzoa pointi nyingi zaidi ndani ya msimu mmoja zikiwa 89.
Tanta, FC Masr na Haras El Hodood zimeshushwa kucheza ligi ya daraja ya kwanza huku mabingwa wa msimu wa mwaka 1972 na 1973 Ghazl El Mahalla wakipandishwa ngazi pamoja na Bank Al Ahly na Ceramica Cleopatra.
TOPSHOT - This picture shows the trophy prior to the draw of the Confederation of African Football's (CAF) Champions league at the Ritz Carlton Hotel in Cairo on December 28, 2018. (Photo by MOHAMED EL-SHAHED / AFP) (Photo credit should read MOHAMED EL-SHAHED/AFP/Getty Images)
Fainali ya kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika itaandaliwa Novemba 27 katika uwanja wa Borg Al Arab Stadium mjini Alexandria,Misri.
Kwa mjibu wa Kamati andalizi ya mashindano hayo ya baina ya vilabu marudio ya nusu fainali ya pili kati ya Zamalek na mabingwa wa Moroko Raja Casablanca itakuwa tarehe 4 Novemba katika uwanja wa kimataifa wa Cairo.
Nusu fainali hiyo ilikuw aipigwe Novemba mosi lakini ikaahirishwa kutokana na wachezaji 11 wa timu ya Casablanca kupatikana na ugonjwa wa Covid 19 na hivyo kuzuiliwa kusafiri hadi Misri na Serikali ya Kifalme ya Moroko.
Zamalek wanaongoza bao 1 kwa bila kutokana na mkumbo wa kwanza huku mshindi akichuana dhidi ya mabingwa mara 8 Al Ahly ambao walitinga fainali kwa ushindi wa jumla ya mabaoa 5-1 katika nusu fainali .
Mechi hizo zimeratibiwa upya kufuatia agizo la chama cha soka nchini Misri ambao ni mwandalizi wa mechi hizo ,kuambatana na masharti ya kimataifa dhidi ya Ugonjwa wa Covid 19.
Mshindi wa kombe hilo atashiriki kombe la dunia baina ya vilabu ,kipute kitakachoandaliwa nchini Qatar kati ya Desemba 11 na 21 mwaka huu kando na zawadi ya Dola Milioni 2 nukta 5.
Mabingwa mara 8 ligi ya mabingwa Afrika Al Ahly ya Misri walitinga fainali ya taji hiyo kwa mara ya 9 baada ya kuwacharaza Wydad Casablanca ya Moroko mabao 3-1 katika marudio ya nusu fainali jijini Cairo Ijumaa Usiku.
Marwan Mohsen na Hussein Elshahat walipachika mabao ya Ahly maarufu kama Red Devils walioenda mapumzikoni kwa ushindi wa mabao 2 -0, kabla ya Yasser Ahmed Ibrahim kuongeza bao la tatu kunako kipindi cha pili kupitia kichwa , naye nguvu mpya Zouheir El Moutaraji akifunga bao la maliwazo kwa wageni.
Ahly wanaofunzwa na kocha Pitso Mosimane kutoka Afrika kusini walifuzu kwa fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-1 ,baada ya kusajili ushindi wa mabao 2-0 katika duru ya kwanza ya nusu fainali wiki jana.
Itakuwa mara ya tisa kwa miamba hao wa Misri kucheza fainali ya kombe hilo la kifahari barani Afrika ,wakijivunia rekodi ya kutoshindwa katika mechi 28 za ligi ya mabingwa Afrika na ushindi wa 17 mtawalia nyumbani .
Ahly watakuwa wakiwania kombe hilo kwa mara ya 9 wakiwa na rekodi ya kutopoteza katika fainali na pia wakiwania kombe hilo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2013, huku kocha Mosimane akiwinda kombe la pili la ligi ya mabingwa Afrika baada ya kulinyakua miaka 4 iliyopita akiwa na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.
Mabingwa wa Misry Al Ahly watukatana kwenye fainali ya Novemba 6 na mshindi wa nusu fainali ya pili baina ya Zamalek ya Misri dhidi ya mabingwa wa Moroko Raja Casablanca ambayo iliahirishwa kutoka Oktoba 24 baada ya wachezaji 8 wa Casablanca kupatikana na Covid 19.
Mabingwa mara nane wa taji ya ligi ya mabingwa Afrika Al Ahly walijiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali ya kombe hilo baada ya kusajili ushindi wa mabao 2-0 ugenini mjini Casablanca dhidi ya wenyeji Wydad Casablanca.
Alhy maarufu kama Red Devils wanaofunzwa na Pitso Mosimane walianza mkondo huo wa kwanza wa semi fainali kwa makeke na matawi ya juu huku Magdi Kafsha akifunga bao la kwanza kwa wageni kunako dakika ya 4 ya mchezo nayo wenyeji wakakosa penati iliyopigwa na Aouk Badi na kupanguliwa na kipa wa Ahly Mohammed
El Shanawy.
Wydad walionekana kupotea mchezoni katika kipindi cha pili ,wageni wakimiliki mpira kwa kipindi kirefu kabla Ali Malooul kufunga bao la pili katika dakika ya 62 kupitia mkwaju wa penati.
Mkondo wa pili wa nusu fainali utasakatwa jijini Cairo Misri wikendi ijayo ambao Ahly wanahitaji tu sare au hata kupoteza kwa bao moja ili kutinga fainali,huku wakiwania taji ya 9.
Mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya pili kuchezwa Jumapili usiku,Raja Casablanca ya Moroko ikiwakaribisha vigogo wa Misri Zamalek,mechi ambapo itarushwa mbashara na Kbc channel 1 Tv.