Safari ya timu ya Gor Mahia kuelekea Algeria imekumbwa na utata baada ya kudaiwa kukosekana kwa ndege ya usafiri moja kwa moja kutoka Nairobi hadi Algiers .
Kogalo walitarajiwa kusafiri Jumapili usiku kwenda Algiers kwa mkumbo wa kwanza wa mechi ya mchujo kuwania ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya mabingwa wa Algeria CR Belouizdad Jumatano jioni ,lakini hadi mapema Jumatatu timu hiyo ilikuwa bado haina uhakika wa kusafiri.
Awali timu hiyo ilikosa tiketi za usafiri kabla ya kampuni Air 748 kutoa shilingi milioni 1 kwa usafiri huku pia yamkini tiketi zilizonunuliwa hazikutosha kwa wachezaji na maafisa wote wanaohitajika kwenye ziara hiyo.
Pia wachezaji wanadai kulipwa mishahara yao kabla ya kusafiri na huenda wakosa kucheza mechi hiyo hatuya ambayo itachangia kupigwa marufuku na kutozwa faini na CAF.
Mkumbo wa pili wa mchuano huo uliratibiwa kuchezwa jijini Nairobi mapema mwezi ujao huku mshindi wa jumla akitinga hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika.