Gambia yawagutusha Ghana huku Tanzania wakitimuliwa AFCON U 20
Gambia ilitoka nyuma na kuwabwaga Ghana magoli 2-1 katika mchuano wa kundi C uliosakatwa Jumatatu usiku nchini Mauritania.
Abdul Fatawualikuwa ameiweka Ghana uongozini baada ya dakika 8 za mchezo ,kabla ya Kajally Drammeh na Lamarana Jallow kuwafungia Young Scorpions magoli 2 na kuwaweka Limbukeni Gambia uongozini kufikia mapumzikoni .
Licha ya kupewa kadi nyekundu Gambia walijizatiti na kutwaa ushindi huo mhimu uliowafuzisha kwa robo fainali wakimaliza wa pili kwa alama 4.
Katika mechi nyingine Moroko waliikomoa Tanzania mabao 3-0 na kuongoza kundi hilo la C El Mehdi El Moubarik, Mohammed Amine Essahel na Ayoub Mouloua wakipachika magoli ya Moroko katika kipindi cha kwanza na kuongoza kundi kwa pointi 7.