Wanamuziki Nandy na Billnass wametengana baada ya uhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu. Mara ya kwanza kwa watu kukisia kwamba mambo sio mazuri, ni wakati Nandy alijitokeza kutangaza kwamba pete ya uchumba aliyovishwa na Billnass ilikuwa imepotea.
Wengi walihisi kwamba Nandy alivua pete hiyo mwenyewe lakini amekuwa akijitetea akisema kwamba alivuliwa na mashabiki bila kujua kipindi cha kutumbuiza kwenye mikutano ya Kampeni mwaka jana.
Mara nyingine ni wakati alikwenda kumlaki mwanamuziki Koffi Olomide kwenye uwanja wa ndege yapata mwezi mmoja uliopita na alikuwa amemwalika kwa ajili ya kufanya kibao naye.
Nandy hakuwa na Billnass jinsi wengi walitarajia lakini Nandy alisema kwamba mpenzi huyo wake alikuwa naye kwenye mipango yote hata ingawa hakuonekana huko kwenye uwanja wa ndege.
Baadaye Nandy na Koffi walitumbuiza tena kwenye tamasha lililokuwa limeandaliwa na Clouds Media kwa ajili ya siku ya wapendanao lakini Billnass hakuonekana huko. Mamake Nandy alipohojiwa siku hiyo alisema mambo kati ya wanawe yalikuwa sawa na alikuwa anasubiri tu wampe siku ya arusi.
Siku ya kuzindua kibao chake na Koffi kwa jina “Leo Leo” kwenye kipindi cha “Leo Tena” cha Clouds Tv Billnass pia hakuonekana na Nandy aliendelea tu kumtetea akisema anamuunga mkono kwa kazi yake.
Nandy mwenyewe alitangaza utengano wake na Billnass wakati alikuwa anajibu shabiki mmoja ambaye alimwita mke wa Billnass kwenye picha aliyopachika kwenye Instagram.
Shabiki huyo kwa jina carinamarapachi aliandika “Mrs Billnass love uu more” naye Nandy akamjibu “Single”.