Armenia leo imeishtumu Uturuki kwa kuzuia ndege zinazosafirisha misaada ya dharura kutumia anga yake.
Azerbaijan na Armenia zimeshtumiana kwa kukiuka mkataba wa kukomesha vita uliopatanishwa chini ya juma moja lililopita ili kuwezesha pande hizo mbili kubadilishana wafungwa na miili ya wale waliouawa kwenye makabiliano yaliyozuka tarehe 27 mwezi uliopita.
Makabiliano hayo ndio mabaya zaidi tangu miaka ya tisni ambapo watu elfu-30 waliuwa kwenye vita kuhusiana na eneo la Nagorno-Karabakh ambalo hutambulika kimataifa kuwa sehemu ya Azerbaijan lakini linalotawaliwa na waarmenia.
Wizara ya Azerbaijan imesema kuwa jeshi lake linaendeleza shughuli zake kwenye mpaka wa Nagorno-Karabakh, lakini ikasema taharuki inazidi kutanda kwenye maeneo ya Aghdere-Aghdam na Fizuli-Hadrut-Jabrail.
Wizara ya Mashauri ya Nchi za Kigeni ya Uturuki ambayo hushughulikia maswala kuhusu anga haikutoa kauli mara moja kuhusu shutma hizo.